MAADHIMISHO YA SARATANI YA MACHO KWA WATOTO (RETINOBLASTOMA)
Ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, inapenda kuwataarifu kuhusu wiki ya maadhimisho ya saratani ya macho kwa watoto itakayoanza tarehe 11/6/2026 hadi 15/6/2026 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi 9:30 alasiri.
Huduma zitakazotolewa;
Elimu ya saratani ya macho kwa Watoto
Uchunguzi wa Saratani ya macho
Uchunguzi wa mtoto wa jicho
Kupima presha ya macho
Uchunguzi wa mzio
Hivyo wote wenye matatizo na wanaohitaji huduma wafike katika uwanja wa Mukendo, Manispaa ya Musoma ili waweze kupata huduma hizo muhimu. Huduma hizi zitatolewa bure.



